![]() |
| Ismail Haki, kutoka shirika la TIKA (kulia) na Gavana wa Garissa, Narthif Jama. |
Gavana wa Kaunti ya Garissa, Nathif Jama, amepuuzilia mbali madai kuwa serikali yake imerudisha bilioni moja nukta mbili ya pesa iliyotengewa na serikali kuu kwa minajili ya maendeleo ya kaunti hiyo.
Akiwahutubia wananchi katika mji wa Garissa baada ya kupokea magari ya kuokota taka yaliyotolewa na shirika la kituruki la TIKA, Jama alijitetea na kusema kuwa waliutumia mgao wao vyema "Kaunti yetu haiwezi ikachukua hatua kama hiyo . Tumezitumia fedha tulizotengewa kufadhili miradi mbalimbali katika kaunti hii", alisema.
Nathif ametofautiana na ripoti hiyo iliyowasilishwa kwa bunge la seneti na msimamizi wa bajeti huku akihoji kuwa serikali yake imeshuhudia upungufu wa fedha kinyume cha madai kuwa haikuweza kutumia fedha ilizotengewa vikamilifu.
Wakati huo huo, Gavana huyo ameishukuru serikali ya uturuki kwa msaada huo huku akiwataka wenyeji wa mji huo kuyatumia magari hayo vyema ili kufanikisha usafi katika mji huo.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa serikali ya Uturuki, Ismail Haki, ameahidi kuwa serikali hiyo itaendelea kuunga mkono miradi ya maendeleo katika kaunti hiyo na serikali ya Kenya.
"Tutaendelea kufanya kazi na wenyeji wa kaunti ya Garissa ili kuboresha maisha yao. Tulikuwa pamoja wakati wa kiangazi na tutazidi kushirikiana nanyi," alimaliza bwana Ismail.
Msaada huo wa magari umepiga jeki hatua za kuleta usafi katika mji huo huku wenyeji wakijawa na matumaini kuwa magari hayo yatatumika vyema.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa serikali ya Uturuki, Ismail Haki, ameahidi kuwa serikali hiyo itaendelea kuunga mkono miradi ya maendeleo katika kaunti hiyo na serikali ya Kenya.
"Tutaendelea kufanya kazi na wenyeji wa kaunti ya Garissa ili kuboresha maisha yao. Tulikuwa pamoja wakati wa kiangazi na tutazidi kushirikiana nanyi," alimaliza bwana Ismail.
Msaada huo wa magari umepiga jeki hatua za kuleta usafi katika mji huo huku wenyeji wakijawa na matumaini kuwa magari hayo yatatumika vyema.




