Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 26 June 2014

Arsenal yawatimua wachezaji kumi na moja


Miamba wa soka nchini uingereza na mabingwa wa Kombe la F.A, Arsenal fc imetangaza rasmi kuwa imetengana na wachezaji kumi na moja wa timu hiyo ili kutoa nafasi kwa wachezaji wanaotaka kuwasajili.

Kupitia taarifa kwenye mtandao wake wa Arsenal.com, mshambulizi matata wa Denmark, Niklas Bendtner na nahodha wa zamani wa Korea kusini J.Y Park wameihama timu hiyo baada ya mkataba wao kumalizika.

Wakati huo huo, wachezaji waliojiunga na timu hiyo kwa njia ya mkopo, Kim Kallstrom wa Sweden na kipa Emiliano Viviano watarejea kwa wamiliki wao baada ya kutumikia mda wao wa mkopo ugani emirates.

Aidha mdakaji Lukasz Fabianski, beki Bacary Sagna na kiungo Zak Ansah wameihama timu hiyo baada ya kudinda kurefusha kandarasi zao an timu hiyo.

Wengine walioigura timu hiyo ni wachezaji chipukizi, Chuks Aneke na Daniel Boateng, Zach Fagan na Leander Siemann.

Kutoka hapa mtitigo, tunawatakia mastaa hao kila la heri popote watakapokwenda kusakata kambumbu.





No comments:

Post a Comment