Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Friday, 21 November 2014

SUPKEM YATAKA WASIMAMIZI WA USALAMA MOMBASA WAONDOLEWE

Viongozi wa baraza kuu la Waislamu nchini Kenya, (Supkem) kutoka kaunti ya Garissa wametoa wito kwa serikali itekeleze mabadiliko kwa wasimamizi wa uslama mjini Mombasa kwa kutowajibika.

Wakizungumza mjini Garissa mapema leo, viongozi hao wakiongozi na Mwenyekiti wa Supkem mjini humo, Abdullahi Salat, wamewalaumu maafisa wakuu wa uslama mjini Mombasa kwa ongezeko la visa vya utovu wa usalama.

"Tunamuomba Rais Uhuru Kenyatta, awafanyie mabadiliko Wakuu wa usalama mjini Mombasa, kwa sababu wengi wao wamekuwa na ukatili dhidi ya wenyeji wanaostahili kuwalinda na hivyo basi kusababisha kutoaminiana", Abdullahi amesema.

Aidha viongozi hao wamelaani vikali hatua ya kufungwa kwa misikiti na kufurushwa kwa waumini mara kwa mara huku wakidai kuwa huenda hali hiyo ikaathiri uwiano mjini humo. Badala yake, viongozi hao wameiri serikali kutumia mbinu mbadala za kupambana na washukiwa wa uhalifu bila kuwalenga waumini.

Vilevile, Abdullahi amewaonya maafisa wa usalama dhidi ya kulenga misikiti huku akieleza kuwa misikiti ni eneo muhimu la ibada wala sio maskani ya wahalifu.

Viongozi hao wa Supkem wameongeza kuwa viongoi wa kidini ndio wanaostahili kulifumbua tatizo linalosibu mjini Mombasa kwa njia ya mazungumzo wala sio kupitia maafisa wa usalama.

Haya yanajiri baada ya maafisa kutoka vikosi mbalimbali vya usalama kuvamia misikiti ya Musa, Sakina na Swafaa na kuwakamata zaidi ya vijana 200.


Kwa sasa, Misikiti hiyo iko chini ya ulinzi mkali huku wenyeji wakilazimika kusaka njia mbadala za kutekeleza Ibada.

Friday, 5 September 2014

Mombasa county unites with Constituencies for development projects

Mombasa county governor Hassan Ali Joho led various leaders from the area including Mps and Mcas on a four day development tour of Kisauni constituency a few days after a similar operation in Jomvu and Changamwe constituencies.

Speaking after commissioning of 2 solar powered boreholes in Mjambere and Magogoni wards which are expected to serve over 5000 people, Joho said the effort was aimed at combining the County’s development agenda with the development plans of various constituencies to improve the living condition Mombasa residents.

“Team work is paramount. I am glad that all levels of leadership in Mombasa County are working together as one compact unit. This is the seed that we planted almost a year ago and now the fruits are clearly visible for our people to benefit from", he said.
The governor also added that the move played a significant role in eliminating duplications and ensuring standardization in all development projects throughout the County.
 
Amongst area leaders who accompanied the  Governor, included Senator Hassan Omar, area Kisauni Mp, Rashid Bedzimba, Jomvu Mp, Badi Twalib.

The team also commissioned the Msikitini Cabro road of 350 meters at the cost of about Kshs 4.5M. 

The governor praised Kisauni Mp Bedzimba for for exhibiting efficiency and transparency in the execution of the project.
 
Joho is expected to lead the commissioning of more projects in Mwakirunge ward on Friday and Junda ward on Saturday.

Thursday, 31 July 2014

Mkufunzi wa Bandari, Twahir Muhiddin alazwa hospitalini

Kocha wa Bandari, Twahir Muhiddin
Kocha Twahir Muhiddin anayewafunza wawakilishi wa pwani katika ligi kuu ya soka humu nchini, Bandari, anaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Mombasa baada ya kuugua.

Akithibitisha taarifa hiyo, meneja wa bandari, Charles Obwaka ameeleza kuwa Twahir amelazwa hospitalini siku ya jumamosi baada ya kupatwa na maumivu.

Obwaka ameongeza kuwa wanamatumaini kuwa Twahir atarejea katika hali ya kawaida na kuendelea kuinoa timu hiyo inayoshikilia nafasi ya kumi na moja kwenye jedwali la ligi kuu ya soka humu nchini.

Kutokuwepo kwa Twahir haikuathiri timu hiyo kwani Bandari ilijitahidi na kuondoka na sare ya goli moja dhidi ya Tusker kwenye mchuano wa ligi ulioandaliwa katika uwanja wa Mombasa siku ya jumapili.

Kufikia sasa manaibu wakufunzi wa Bandari, Ali Breik na Nassoro Mwakoba wanaendelea kuifunza timu hiyo kwa minajili ya mchuano wake wa ligi ugenini dhidi ya Mathare itakayochezwa tarehe sita mwezi ujao.

Gavana Joho amtimua waziri wa fedha, Walid Khalid

Aliyekuwa waziri wa fedha, kaunti ya Mombasa, Walid Khalid
Baada ya vuta nikuvute kati ya bunge la kaunti ya Mombasa na waziri wa Fedha, Walid Khalid, hatimaye Gavana wa Mombasa Hassan Ali Joho amemuachisha kazi waziri wake wa fedha, Walid Khalid.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, Joho amekariri kuwa amechukua hatua hiyo baada ya misururu ya Khalid kukumba na madai ya ukiukaji wa sheria za utoaji zabuni na ununuzi wa mahitaji ya serikali ya  kauti ya Mombasa.

Awali wabunge wa kaunti ya Mombasa waliwasilisha hoja ya kutokuwa imani na Khalid huku wakidai kuwa hawajapendezwa na utendakazi wake.

Kwa sasa Gavana Joho amemteua waziri wa vijana na michezo, Hazel Koitaba kuwa kaimu waziri wa fedha huku gavana huyo akisubiriwa kumteuwa waziri mpya wa fedha.



Uanzilishi wa taa za trafiki Mombasa, zapongezwa

Taa za trafiki zikimulika barabarani

Wamiliki wa magari ya uchukuzi mjini Mombasa wameipongea serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kufanikisha taa za trafiki.

Wakiongozwa na mfanyibiashara maalum,na mmiliki wa kampuni moja ya mabasi, Mohamed Ibrahim, wafanyibiashra hao wameeleza kuwa taa hizo zimepunguza ajali za barabara pamoja na msongamano wa magari mjini Mombasa.

Kwa upande wake waziri wa uchukuzi mjini Mombasa, Mohamed Abbass, ametoa ufafanuzi kuwa serikali ya kaunti hiyo imechukua hatua hiyo kama njia moja ya kuimarisha sekta ya uchukuzi mjini humo.

Abbass ameongeza kuwa serikali hiyo inalenga kuzidisha idadi ya taa hizo katika maeneo mengine mjini humo ili kuzuia msongamano wa magari na ukiukaji wa sheria za barabarani.

Taa hizio zimewekwa katika barabara mbalimbali kama vile, Buxton, Digo na Sabasaba.





Viongozi wa Mombasa wataka miraa ipigwe marufuku

Zao la miraa linalotaka kupigwa marufuku
Viongozi mbalimbali mjini Mombasa, wameapa kuhakikisha kuwa zao la miraa limepigwa marufuku mjini humo huku wakiilaumu kwa uzembe na kudorora kwa afya ya wakazi wa mji huo.

Wakiongozwa na mbunge wa Changamwe, Omar Mwinyi na mwenzake wa Jomvu, Badi Twalib, na wabunge mbalimbali wa kaunti, viongozi hao wamemrai gavana wa mombasa, Hassan Ali Joho, apige marufuku uuzaji na utumizi wa miraa huku viongozi hao wakidai kuwa idadi kubwa ya wenyeji wa kaunti hiyo wameathirika pakubwa na matumizi ya zao hilo huku mamilioni ya fedha zikitumika kwa ununuzi wake.

Kwa upande wao wabunge wa kaunti wametoa wito kwa wabunge wenzao waunge mkono mpango huo huku wakihoji kuwa hatua hiyo itakuw ana manufaa makubwa kwa maendeleo ya kaunti hiyo.

Kauli ya viongozi hawa inajiri wiki chache tu baada ya bunge la kaunti ya Mombasa kupinga mswada dhid ya miraa uliowasilishwa na mwakilishi wa wodi mteule, Fatma Swaleh.

Madereva wengi mjini Mombasa wamelaumiwa kwa kuendesha magari wakitumia miraa huku wakihatarisha maisha ya maabiria.

Hata hivyo mamlaka ya kitaifa ya kudhibiti vileo na mihadarati, Nacada, imeambia serikali ya kaunti ya mombasa iuende sheria itakayoongoza juu ya uuzaji na utumiaji wa miraa katika maeneo muhimu mjini humo.

Mtalii wa Kijerumani auwawa Mombasa

Watalii wakiwasili humu nchini
Taharuki imetanda mjini Mombasa baada ya mtalii mmoja kutoka Ujerumani kuuwawa kwa kupiga risasi katika mtaa wa Mji wa Kale, mjini Mombasa usiku wa kuamkia leo.

Mtalii huyo, ChristineTex mwenye umri wa miaka 30, alifariki papo hapo baada ya watu waliojihami kwa bnduki kuwamiminia risasi yeye pamoja na mchumba wake, Henri Sekandi.

Kulinga na mkuu wa idara ya polisi wa utalii, mjini Mombasa,Robert Sicharani, mwanamke huyo alikuwa pamoja na mchumba wake kutoka Uganda huku wawili hao wakiwa katika ziara ya kitalii katika mji wa kihistoria wa Mji wa kale.

Kwa upande wake, Khalid Ibrahim, ambaye ni msimamizi wa polisi jamii katika mtaa wa mji wa kale, ameeleza kuwa mwanamke huyo aliuwawa bila kuibiwa chochote huku kiini cha mauaji yake kikisalia kuwa kitendawili.

Mji wa Kale umekuwa ukishuhudia mauaji ya watalii ya mara kwa mara kwani miezi michache iliyopita, watalii watatu kutoka urusi walishambuliwa na kuuwawa kwa kupigwa risasi.

Polisi wanaendeleza uchunguzi ili kubaini chanzo cha mauaji hayo.