Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 26 June 2014

Chuo kikuu cha Technical University of Mombasa chafungwa






















Shughuli za masomo zimekatizwa katika tawi kuu la chuo kikuu cha kiufundi cha Mombasa  kufuatia mgomo wa wanafunzi wa chuo hicho.

Wanafunzi wa kozi za uhandisi wanadaiwa kuanzisha mgomo huo huku wakidai kuwa chuo hicho hakina uwezo wa kutoa kozi hiyo na badala yake sasa wanataka wahitimu kozi hiyo katika chuo kikuu cha kilimo na teknolojia Jomo kenyatta.

Hata hivyo wanafunzi hao hawajasababisha uharibifo wowote licha ya maafisa wa polisi kuingilia kati na kuufurusha mgomo huo kwa kutumia vitoa machozi.

Kwa sasa wasimamizi wa chuo hicho wanaendelea na mazungumzo kwenye mkutano wa dharura ili kulifumbua tatizo hilo.

Wanafunzi wote wa chuo hicho wamepewa ilani ya kuondoka haraka iwezekananvyo hadi pale watakapofahamishwa tarehe mpya ya kufunguliwa kwa chuo hicho.


No comments:

Post a Comment