![]() |
| Gavana wa Kaunti ya Lamu, Issa Timamy. |
Gavana Timamy alikamatwa mjini Mombasa siku ya Jumatano na maafisa wa idara ya upelelezi ya CID na kuzuiliwa katika afisi za idara hiyo kwa saa kadhaa ili kuhojiwa.
Kaunti ya Lamu imekuwa chini ya kurunzi kali ya serikali kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara yaliyotekelezwa na watu wasiojulikana na kuwa tishio kubwa kwa usalama wa wenyeji wa kaunti hiyo.
Hata hivyo chanzo cha mauaji katika kaunti hiyo hakijabainika kufikia sasa licha ya Rais Uhuru Kenyatta kueleza kuwa uvamizi katika eneo la mpeketoni lilichochewa kisiasa.
Kundi la wanamgambo la Al Shabaab lilijitokeza na kukiri kuwa lilitekeleza shambulizi la eneo la Mpeketoni huku kundi hilo likiitaka serikali iwaondoe wanajeshi wake walioko nchini Somalia.
Timamy aliponea na kusalia kuwa gavana mnamo mwezi Novemba mwaka uliopita baada ya mahakama ya rufaa kufutilia mbali uchaguzi mdogo wa ugavana ulioratibiwa kufanywa na tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC.

No comments:
Post a Comment