Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 31 July 2014

Mtalii wa Kijerumani auwawa Mombasa

Watalii wakiwasili humu nchini
Taharuki imetanda mjini Mombasa baada ya mtalii mmoja kutoka Ujerumani kuuwawa kwa kupiga risasi katika mtaa wa Mji wa Kale, mjini Mombasa usiku wa kuamkia leo.

Mtalii huyo, ChristineTex mwenye umri wa miaka 30, alifariki papo hapo baada ya watu waliojihami kwa bnduki kuwamiminia risasi yeye pamoja na mchumba wake, Henri Sekandi.

Kulinga na mkuu wa idara ya polisi wa utalii, mjini Mombasa,Robert Sicharani, mwanamke huyo alikuwa pamoja na mchumba wake kutoka Uganda huku wawili hao wakiwa katika ziara ya kitalii katika mji wa kihistoria wa Mji wa kale.

Kwa upande wake, Khalid Ibrahim, ambaye ni msimamizi wa polisi jamii katika mtaa wa mji wa kale, ameeleza kuwa mwanamke huyo aliuwawa bila kuibiwa chochote huku kiini cha mauaji yake kikisalia kuwa kitendawili.

Mji wa Kale umekuwa ukishuhudia mauaji ya watalii ya mara kwa mara kwani miezi michache iliyopita, watalii watatu kutoka urusi walishambuliwa na kuuwawa kwa kupigwa risasi.

Polisi wanaendeleza uchunguzi ili kubaini chanzo cha mauaji hayo.

No comments:

Post a Comment