Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 31 July 2014

Viongozi wa Mombasa wataka miraa ipigwe marufuku

Zao la miraa linalotaka kupigwa marufuku
Viongozi mbalimbali mjini Mombasa, wameapa kuhakikisha kuwa zao la miraa limepigwa marufuku mjini humo huku wakiilaumu kwa uzembe na kudorora kwa afya ya wakazi wa mji huo.

Wakiongozwa na mbunge wa Changamwe, Omar Mwinyi na mwenzake wa Jomvu, Badi Twalib, na wabunge mbalimbali wa kaunti, viongozi hao wamemrai gavana wa mombasa, Hassan Ali Joho, apige marufuku uuzaji na utumizi wa miraa huku viongozi hao wakidai kuwa idadi kubwa ya wenyeji wa kaunti hiyo wameathirika pakubwa na matumizi ya zao hilo huku mamilioni ya fedha zikitumika kwa ununuzi wake.

Kwa upande wao wabunge wa kaunti wametoa wito kwa wabunge wenzao waunge mkono mpango huo huku wakihoji kuwa hatua hiyo itakuw ana manufaa makubwa kwa maendeleo ya kaunti hiyo.

Kauli ya viongozi hawa inajiri wiki chache tu baada ya bunge la kaunti ya Mombasa kupinga mswada dhid ya miraa uliowasilishwa na mwakilishi wa wodi mteule, Fatma Swaleh.

Madereva wengi mjini Mombasa wamelaumiwa kwa kuendesha magari wakitumia miraa huku wakihatarisha maisha ya maabiria.

Hata hivyo mamlaka ya kitaifa ya kudhibiti vileo na mihadarati, Nacada, imeambia serikali ya kaunti ya mombasa iuende sheria itakayoongoza juu ya uuzaji na utumiaji wa miraa katika maeneo muhimu mjini humo.

No comments:

Post a Comment