![]() |
| Kocha wa Bandari, Twahir Muhiddin |
Akithibitisha taarifa hiyo, meneja wa bandari, Charles Obwaka ameeleza kuwa Twahir amelazwa hospitalini siku ya jumamosi baada ya kupatwa na maumivu.
Obwaka ameongeza kuwa wanamatumaini kuwa Twahir atarejea katika hali ya kawaida na kuendelea kuinoa timu hiyo inayoshikilia nafasi ya kumi na moja kwenye jedwali la ligi kuu ya soka humu nchini.
Kutokuwepo kwa Twahir haikuathiri timu hiyo kwani Bandari ilijitahidi na kuondoka na sare ya goli moja dhidi ya Tusker kwenye mchuano wa ligi ulioandaliwa katika uwanja wa Mombasa siku ya jumapili.
Kufikia sasa manaibu wakufunzi wa Bandari, Ali Breik na Nassoro Mwakoba wanaendelea kuifunza timu hiyo kwa minajili ya mchuano wake wa ligi ugenini dhidi ya Mathare itakayochezwa tarehe sita mwezi ujao.

No comments:
Post a Comment