Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 31 July 2014

Uanzilishi wa taa za trafiki Mombasa, zapongezwa

Taa za trafiki zikimulika barabarani

Wamiliki wa magari ya uchukuzi mjini Mombasa wameipongea serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kufanikisha taa za trafiki.

Wakiongozwa na mfanyibiashara maalum,na mmiliki wa kampuni moja ya mabasi, Mohamed Ibrahim, wafanyibiashra hao wameeleza kuwa taa hizo zimepunguza ajali za barabara pamoja na msongamano wa magari mjini Mombasa.

Kwa upande wake waziri wa uchukuzi mjini Mombasa, Mohamed Abbass, ametoa ufafanuzi kuwa serikali ya kaunti hiyo imechukua hatua hiyo kama njia moja ya kuimarisha sekta ya uchukuzi mjini humo.

Abbass ameongeza kuwa serikali hiyo inalenga kuzidisha idadi ya taa hizo katika maeneo mengine mjini humo ili kuzuia msongamano wa magari na ukiukaji wa sheria za barabarani.

Taa hizio zimewekwa katika barabara mbalimbali kama vile, Buxton, Digo na Sabasaba.





No comments:

Post a Comment