Habari za kuaminika kutoka maeneo ya pwani na kaskazini mashariki mwa Kenya

Thursday, 3 July 2014

Mwezi wa Ramadhan yawanufaisha wanabiashara Mombasa

Muuzaji akiwa na mteja kwenye kibanda cha kuuza vyakula

















Wafanyibiashara wa Mombasa wanaendelea kufurahia mapato ya uuzaji wa bidhaa mbalimbali kwenye mwezi wa ramadhan huku waumini wa kiislamu wakitekeleza ibada ya saum.

Wafanyibiashara wa soko la Markiti, mwembe tayari na soko kuu la kongowea wameshuhudia ongezeko la wateja huku biashara zao zikipigwa jeki na hatua ya serikali ya kaunti ya Mombasa ya kuondoa marufuku kwa wachuuzi wa vyakula katika maeneo ya kibiashara mjini humo.

Wengi wa Wafanyibiashara wanaoendelea kunufaika ni wauzaji wa vyakula na vifaa vya nyumbani huku ongezeko la bei za bidhaa hizo likishuhudiwa kutokana na maandalizi ya mlo wa kufungua saumu jioni wa iftar na mlo wa mwisho wa usiku wa daku na waumini wa kiislamu.

Tende, madafu, unga, matunda, mboga na nyama ni baadhi ya bidhaa zenye mvuto mkubwa kwa wateja hao kutokana na umuhimu wa bidhaa hizo katika mwezi wa Ramadhan.

Waumini hao wa kiislamu hutekeleza ibada ya saum ya siku 29 au 30 kila mwezi wa tisa katika kalenda ya kiislamu.


No comments:

Post a Comment